Shughuli Zetu

       SHUGHULI ZA SHIRIKA LA FLCAD
    Shirika linafanya shughuli zinazohusiana na:-
  •        KILIMO
Shirika linatoa elimu juu ya kilimo bora hasa katika  matumizi endelevu ya ardhi, Kilimo hifadhi naUtumiaji wa mbegu bora.
  •     UHIFADHI MAZINGIRA
Shirika linatoa elimu juu ya utunzaji wa Mazingira kwa kutoa mbegu za miti na miche ya miti aina mbali mbali na mafunzo juu ya uanzishaji  na utunzaji wa vitalu vya miche ya miti na upandaji. Pia linatoa elimu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kuhimiza kutokuchoma moto ovyo, kutokata miti ovyo, kupunguza matumizi ya mkaa na kuni,  katika kipengele hiki shirika linawezesha jamii kutengeneza na kutumia majiko banifu ya mkaa na kuni, Matumizi ya Nishati mbadala (Solar energy na Biogas), Shirika pia linawezesha  jamii juu ya utunzaji wa vyanzo vya maji.

Pia shirika limeanzisha vikundi vya Mazingira mashuleni (Environmental school club) katika mashule watoto wanafundishwa utunzaji wa mazingira, Uanzishaji wa miradi ya bustani za mboga mboga na matunda, Mabadiliko ya tabia nchi na jinsi ya kuyakabili
  • UFUGAJI
Shirika linatoa elimu juu ya ufugaji rafiki wa mazingira kwa kuelimisha jamii kufuga mifugo michache yenye tija, Pia shirika linatoa nguruwe, kuku na mbuzi kwa jamii ili waweze kupata  mbolea, lishe na kipato katika kaya
  • AFYA
Shirika linatoa elimu ya lishe kwa jamii kwa kutoa mbegu za mboga mboga na matunda,pia linatoa elimu ya magonjwa mbali mbali ikiwemo Maralia, UKIMWI na  Virusi vya UKIMWI kwa jamii pia  kusambaza vifaa kinga.
  • UJASILIAMALI
Shirika linatoa elimu juu ya  uibuaji/utambuzi wa fursa katika maeneo jamii iliko, uanzishaji wa miradi  ya uzalishaji kama vile ufugaji wa Samaki, kuku, Nyuki, Mbuzi, Bustani za boga boga na matunda  na Uuzaji wa miche ya miti. Pia shirika linawezesha uundaji na uendelezaji wa vikundi vinavyojishughulisha na shughuli mbali mbali ikiwemo uzalishaji na masoko, kuweka na kukopa kwa kutoa elimu na vifaa.









Where tree grow people grow

 

FLCAD DOCUMENTS